Leviticus 10:1-3

Kifo Cha Nadabu Na Abihu

1 aNadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu. 2 bHivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana. 3 cKisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema:

“ ‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia
nitajionyesha kuwa mtakatifu;
machoni pa watu wote
nitaheshimiwa.’ ”
Aroni akanyamaza.

Copyright information for SwhNEN